Wapiga picha wa Clouds Tv wakiwa kazini katika viwanja vya posta,kijitonyama jioni hii kwenye riheso ya wasanii wakijiandaa kwa ajili ya tamasha la fiesta one love
Mkurugenzi wa utafiti na maendeleo Clouuds Media Group Ruge Mutahaba akifuatilia kwa makini namna wasanii wanavyojifua leo jioni
Daa kama utakuwa unawakumbuka vyema ni wasanii waliowahi kutamba sana na wimbo wao nakuhitaji,Sarah na Caz T wakiwa wamepozi wakifuatilia kwa makini maelekezo kadhaa yaliyokuwa yakitolewa kuhusiana na mpangilio mzima wa fiesta.
Toka Kulia ni Baby Madaha,Mr Brue pamoja na Dogo Hamidu wakiwa ndani ya viwanja vya posta,Kijitonyama,mahali ambapo tamasha la fiesta litafanyika kesho kutwa.
Wasanii kibao walikuwepo jioni ya leo kwenye riheso yao
Swaga za watoto wa mjengoni,shoto Shadee,Romeo na Dj Fetty katika pozi safi kabisa jioni hii
Dj Fetty akiwa amepozi na wasanii mahiri katika miondoko ya muziki wa R&B Makamua na Qj
Vichwa vitatu makini kabisa katika anga ya muziki wa bongofleva kutoka THT,kulia ni Barnaba Pipi na Amin wakiwa wamepozi mapema leo jioni kwenye viwanja vya posta,kijitonyama.
Mojawapo ya Screen ikiwa imekamilika
Screen zikiendelea kuwekwa sawa na wataalamu
Baadhi ya taa zitakazo sambazwa kila kona ya kiota cha Fiesta one love siku ya siku ikifika itakuwa kama mchana vile
.jpg)

Maandalizi ya ujenzi wa jukwaa la Fiesta One Love unaendelea safi kabisa katika viwanja vya posta, kijitonyama jijini Dar,kama ukilitazama kwa umakini mwana Jamvini nadhani unaanza kupata picha halisi ya jukwaa hilo litakuwa vipi,sio mbaya kama utaamua kwenda kushangaa kimtindo likiishakamilika kabla ya siku yenyewe.
Mratibu wa Miss Tanzania Uncle Hashim Lundenga akiweka saini kwenye gari aina ya Mitsubishi pajero linalotarajiwa kutolewa kwa mshindi wa bahati nasibu kwenye tamasha la Fiesta One Love, itakayofanyika sambamba na tamasha hilo litakalofanyika kwenye viwanja vya posta Kijitonyama, mashabiki watapata nafasi ya kushiriki katika bahati nasibu hiyo kutokana na tiketi zao walizokata ili kuingia kwenye tamasha hilo ambapo wasanii mbalimbali watatoa burudani kutoka hapa nchini na nje ya nchi akiwemo mkali wa Hiphop kutoka nchini MarekaniBusta Rymes.
Mratibu wa Miss Tanzania Uncle Hashim Lundenga akijaribu kutafuta mahali pa kupiga chata lake kwenye gari la bahati nasibu ya Fiesta One love 2009.
Meneja huduma kwa jamii wa kampuni ya simu za mikononi ya Zain Tunu Kavishe akisisitiza jambo kwa watumiaji wa mtandao wa Zain katika kilele cha tamasha la Fiesta one love.
Meneja huduma kwa jamii wa kampuni ya simu za mikononi ya Zain Tunu Kavishe akimkabidhi mtangazaji wa Clouds Fm Ephrahim Kibonde (kwa niaba ya Clouds Media Group),makao makuu ya Zain,kifurushi kama zawadi/hisani kwa ajili ya kuwapa watoto yatima na waishio katika mazingira magumu,huo ukiwa katika mchakato mzima wa kauli mbiu ya FIESTA HISANI,mchakato huo umefanyika jana ikiwa ni sehemu ya kuelekea kwenye kilele cha tamasha hilo.Kampuni ya Zain ni moja ya wadhamini wa tamasha la fiesta one love linalotarajia kufanyika keshokutwa,jumamosi katika viwanja vya posta,kijitonyama jijini Dar.







Watangaji wa Mjengoni Redio Clouds Zamaradi Mketema kushoto na Ephraim Kibonde katikati wakifanya mahojiano mafupi leo asubuhi na Meneja uhusiano wa Serengeti Breweriers Teddy Mapunda (ambao ndiyo wadhamini wakuu) kuhusiana na maandalizi ya tamasha Fiesta litakalofanyika Novemba 21 katika viwanja vya Posta Kijitonyama, kulia ni meneja matukio wa kampuni hiyo Bahati Singh.
Meneja Uhusiano wa Serengeti Breweriers Teddy Mapunda akiweka saini kwenye gari aina ya Mitsubishi pajero linalotarajiwa kutolewa kwa mshindi wa bahati nasibu kwenye tamasha la Fiesta One Love, itakayofanyika sambamba na tamasha hilo litakalofanyika kwenye viwanja vya posta Kijitonyama, mashabiki watapata nafasi ya kushiriki katika bahati nasibu hiyo kutokana na tiketi zao walizokata ili kuingia kwenye tamasha hilo ambapo wasanii mbalimbali watatoa burudani kutoka hapa nchini na nje ya nchi akiwemo mkali wa Hiphop kutoka nchini Marekani
Miss Utalii katika pozi
Wamenyooka na wanafaa kuwa mabalozi wa utalii wa ndani,lakini mmoja wao ndiye atakayeibuka na taji la Miss utalii kinondoni 2009.
Washiriki wa Miss Utalii Kinondoni -2009 wakiwa wamejiachia katika mapozi mbalimbali kando kando ya fukwe za COCO Beach, mwishoni mwa wikend.shindano la Miss Utalii Kinondoni linatarajia kufanyika Novemba 20 katika ukumbi wa Msasani Club kinondoni jijini dar.
Baadhi ya washindi wa Boom club waliojishindia tickets, wakiwa katikaPicha ya pamoja walipokabidhiwa vitambulisho vyao vya kuingilia katika hafla hiyo Iliyohudhuriwa na marais mbalimbali kutoka Africa 
Mwanamuziki nyota wa kimataifa toka nchini Senegal, Youssou Nd'our akizawadiwa fulana na Mkurugenzi wa Clouds Media Group / Prime Time Promotions Bw.Joseph Kusaga mchana huu.
Mkuu wa vipindi wa Choice Fm ML Chris akiwa amepozi na Youssou Nd'our
Youssou Nd'our akifafanua jambo kwa msisitizo mkubwa kabisa
watangazaji wa Choice Fm Thandy na Baby Kabaye wakizungumza na Youssou Nd'our leo mchana
Youssou Nd'our akifanya mahojiano mafupi leo mchana ndani ya redio ya Choice Fm,pichani ni watangazaji Baby Kabaye na Thandy.Mwanamuziki huyo amesema kuwa amefurahishwa sana na onesho lake la usiku wa kuamkia leo ambalo anakiri wazi kuwa muziki wake unakubalika kwa kiasi kikubwa ikiwemo Tanzania,Youssou Nd'our amesema kuwa anatarajia kurejea tena nchini Tanzania Januari mwakani kwa shughuli maalumu.
Unaona bwaana,huu ndiyo mpango mzima.! Mtangazaji wa kipindi cha XXL akipeana mkono na Youssou Nd'our kulia kabisa ni Bakari wa Marketing na nyuma kabisa ni Dj Mully B
"Na hii ni studio yetu ya pili ambayo itakuwa ikiendeshwa kisasa kabisa,mara baada ya kila kitu kukamilisha muda mfupi ujao"Sebastian Maganga akimueleza Youssou Nd'our leo mchana
Youssou Nd'our akiimba kwa hisia jukwaani
Mwanamuziki Angelique Kidjo kutoka nchini Benin akiimba kwa hisia
Mashabiki wakijiwaya mwaya jukwaani safi kabisa
Youssou Nd'our na Angelique Kidjo wakiimba kwa pamoja jukwaani mbele ya umati mkubwa wa watu katika onesho lililofanyika usiku wa kumkia viwanja vya Karimjee.
Youssou Nd'our V/S Angelique Kidjo palikuwa hapatoshi jukwaaani ohoo.
Mwanamuziki nyota wa kimataifa toka nchini Senegal, Youssou Nd'our akitumbukiza kwenye onesho viwanja vya karimjee jijini dar usiku wa kuamkia leo.
Mwanamuziki mwenye asili ya Sudan anayeishi Misri, Emmanuel Jah, akitambulishwa rasmi mbele ya mashabiki kibao na Mwanamuziki nyota wa kimataifa toka nchini Senegal, Youssou Nd'our wakati wa onesho lililofanyika katika viwanja vya karimjee usiku wa kuamkia leo.
"Mzuka ukipanda bwana hauzuiliki hata kidogo"! Pichani ni mwanamuziki nyota wa Kimataifa kutoka nchini Benin, Angelique Kidjo akionesha umahiri wake wa kucheza jukwaani,huku mashabiki waliokuwemo viwanjani hapo walikuwa hawaishi mayowe ya shangwe.
Mashabiki kibao katika viwanja vya Karimjee wakati nyota wa muziki wa kimataifa walipokuwa wakitumbuiza usiku wa kuamkia leo,jijini dar.Onesho hilo ambalo lilifana sana liliratibiwa na kampuni bingwa ya burudani hapa nchini ya Prime Time Promotions Ltd na kudhaminiwa nakampuni ya simu za mikononi ya Zain.
Pasha akiwasha moto katika fiesta one love Zanzibar ndani ya ngome kongwe
Baadhi ya mashabiki waliojitokeza katika fiesta one love 2009 Zanzibar
Kikundi cha Stone town kikionyesha umahiri wake wa kucheza nyimbo za mahadhi ya kihindi
Hata akina dada hawakuwa nyuma kuonyesha vipaji vyao vya kujiachia
Alikiba akiwapagawisha mashabiki wake na wimbo wake wa msiniseme
Mashabiki wakijiachia ndani ya fiesta one love 2009 Zanzibar
Chama kubwa Tip Top conection wakiwasha moto ... kutoka kulia ni Tunda Man, Khasim na Madee kifiesta fiesta
Kundi linalopendwa Zanzibar ndani ya Zenji Offside Trick a.k.a Wazee wa samaki wakishoo love
Dj Dr. B akiwasha moto ndani fiesta one love 2009
Kijana machachali aitwaye Wasi kutoka Clouds Tv wakishow love ndani ya fiesta one love 2009 Zanzibar
Baby J akionyesha umahiri wake wa kucheza na kuimba katika fiesta one love 2009 Zanzibar
Michael Jackson bado anakumbukwa Zenji,kama uonavyo pichani msanii kutoka Zanzibar akionesha umahiri wake wa kuyarudi mangoma ya The Wacko jacko ndani ya tamasha la fiesta one love
Kikundi cha vijana machachari kutoka Zanzibar wakitumbuiza jukwaani
Youssour Nd'our wakiimba kwa pamoja kwa hisia na Angelique Kidjo ndani ya Mlimani CityWarembo wanaoshiriki mashindano ya kimataifa ya MISS EAST AFRICA 2009 wataanza kuwasiri Nchini tarehe moja mwezi ujao kwa ajili ya mashindano hayo yanayosubiliwa kwa hamu kubwa na watu wengi Barani Afrika.
Wakiwa jijini Dar es salaam, warembo hao watafikia katika hoteli ya kimataifa ya Kunduchi Beach Hotel & Resort ambayo ndiyo hoteli rasmi ya mashindano ya Miss East Africa 2009.
Mashindano ya MISS EAST AFRICA 2009 yanatarajiwa kufanyika tarehe 18 mwezi ujao katika ukumbi wa Mlimani City jijini dare s salaam na yatawashirikisha warembo kutoka Nchi 14 za ukanda wa Afrika mashariki ambazo ni pamoja na wenyeji Tanzania,
Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.
Nchi zingine zinazoshiriki katika mashindano hayo ni Ethiopia, Eritrea, Djibouti, Somalia, pamoja na visiwa vya Seychelles, Comoros, Madagascar, Reunion na Mauritius.
Mashindano hayo yanayoandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Limited ya jijini Dar es salaam yanatarajiwa kutizamwa na watu zaidi ya millioni 200 kupitia katika Television barani Afrika.
Mrembo Claudia Niyonzima wa Burundi ndiye anayeshikilia taji la Miss East Africa kwa sasa.
Rena Callist,
Chairman,
MISS EAST AFRICA PAGEANT