SCHOLARSHIP FORUM

Friday, November 20, 2009
Napenda kuwatangazia ndugu wadau wote kuhusu maboresho niliyoweka katika mtandao kuhusiana na mambo ya scholarships.
Nimeanzisha SCHOLARSHIP FORUM ambayo ni www.scholarshipnetwork.ning.com
Hii ukijiunga itakusaidia kupata updates za kila scholarship info ninayoiweka katika link hiyo. Kila tangazo la scholarship niki-post hapo utapata e-mail kukujulisha.
Pia blog www.makulilo.blogspot.com nayo itaendelea kuwa hewani kama kawaida.
Mdau MAKULILO, Jr.
San Diego, CA
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 20, 2009 | | Permalink | Maoni 3

taarifa ya msiba mbeya

Dada Alice J.B. Kibopile (Alice Ngubwene) anasikitika kutangaza kifo cha baba yake mzazi mpendwa,John Burton Kibopile wa Forest Mbeya,kilichotokea jana tar 19/11/2009 asubuhi katika hospitali ya rufaa Mbeya.
Marehemu Jonh ampaka anafariki alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa w shinikizo la damu na kisukari.Aidha mazishi yamepangwa kufanyika nyumbani kwake Forest,Mbeya siku ya jumamosi (kesho) tarehe 21/11/2009.
Kwa taarifa zaidi wasiliana na
Paul 0754294999,
Patrick 0784255413,
Alice 07i6501676/0733606
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 20, 2009 | | Permalink | Maoni 0

mchakato mzima wa riheso la fiesta jioni hii

Thursday, November 19, 2009
Wapiga picha wa Clouds Tv wakiwa kazini katika viwanja vya posta,kijitonyama jioni hii kwenye riheso ya wasanii wakijiandaa kwa ajili ya tamasha la fiesta one love
Mkurugenzi wa utafiti na maendeleo Clouuds Media Group Ruge Mutahaba akifuatilia kwa makini namna wasanii wanavyojifua leo jioni
Daa kama utakuwa unawakumbuka vyema ni wasanii waliowahi kutamba sana na wimbo wao nakuhitaji,Sarah na Caz T wakiwa wamepozi wakifuatilia kwa makini maelekezo kadhaa yaliyokuwa yakitolewa kuhusiana na mpangilio mzima wa fiesta.
Toka Kulia ni Baby Madaha,Mr Brue pamoja na Dogo Hamidu wakiwa ndani ya viwanja vya posta,Kijitonyama,mahali ambapo tamasha la fiesta litafanyika kesho kutwa.
Wasanii kibao walikuwepo jioni ya leo kwenye riheso yao
Swaga za watoto wa mjengoni,shoto Shadee,Romeo na Dj Fetty katika pozi safi kabisa jioni hii
Dj Fetty akiwa amepozi na wasanii mahiri katika miondoko ya muziki wa R&B Makamua na Qj
Vichwa vitatu makini kabisa katika anga ya muziki wa bongofleva kutoka THT,kulia ni Barnaba Pipi na Amin wakiwa wamepozi mapema leo jioni kwenye viwanja vya posta,kijitonyama.
Wako safi kwa hiyo safi.

Watoto wa mjengoni na swaga lao kimtindo,toka shoto ni Arnold Kayanda a.k.a Afande Nzabolimana,Dina Marios,Shadee,Dj Fetty,Zamaradi pamoja na Romeo.


Shoto ni Suka akiwa amepozi na wasanii waliofika kwenye riheso yao leo jioni
Baadhi ya wasanii kutoka THT wakiwa wamepozi mapema leo jioni katika viwanja vya posta,kijitonyama jijini Dar walipokuwa wakisubiri kufanya riheso ikiwa ni sehemu ya kujiandaa na tamasha la Fiesta One Love 2009.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 19, 2009 | | Permalink | Maoni 1

Kombe la Dunia la fifa na Coca-Cola lawasili nchini leo


Rais Jakaya Kikwete akiwa ameshikilia Kombe la Dunia la Mpira wa miguu baada ya kuwasili leo katika uwanja wa taifa jijini Dar . Hii ni mara ya pili kwa rais Kikwete kulipokea kombe hilo hapa nchini.
Kombe la Dunia la fifa na Coca-Cola limewasili jioni hii na kupelekwa moja kwa moja kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kombe hilo liliwasili nchini majira ya saa 10:30 jioni na kupokelewa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Joel Bendela kwenye Uwanja wa Ndege wa Mwl Nyerere kabla ya kuelekea Uwanja wa Taifa.Picha kwa hisani ya Father Kidevu
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 19, 2009 | | Permalink | Maoni 1

maandalizi ya fiesta one love ya lala salama


Mojawapo ya Screen ikiwa imekamilika
Screen zikiendelea kuwekwa sawa na wataalamu
Baadhi ya taa zitakazo sambazwa kila kona ya kiota cha Fiesta one love siku ya siku ikifika itakuwa kama mchana vile
Wadau wakifunga screen za kisasa kabisa ambazo zitasambaa kila mahali ndani ya kiota cha fiesta one love
Mitwango ya sauti ikiwa bado iko chini ikisubiri kupandishwa na winchi juu kabisa ya jukwaa
Taa za jukwaani zikiwa bado zimelala doro,zinasubiriwa kupandishwa juu kabisa ya jukwaa.
Taa za jukwaa zikipandishwa leo jioni


Maandalizi ya tamasha la Fiesta one love katika viwanja vya Posta,Kijitonyama bado yanaendelea kwa kasi kubwa,kama uonavyo pichani watu wako bize leo jioni katika kukamilisha kila kitu na kuhakikisha kinakwenda sawa.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 19, 2009 | | Permalink | Maoni 1

sauti za busara zaanza kuwika taratiiibu




Mtanange wa saba wa tamasha la Sauti za Busara ambalo hufanyika Zanzibar kila mwaka itakuwa ni kuanzia tarehe 11 hadi 16 Februari 2010; hakutakuwa na kiingilio kwa watakaoingia kabla ya saa kumi na moja. Sauti za Busara ni tamasha la kimataifa ambalo linautambulisha na kuutangaza muziki wa Afrika Mashariki, na ambalo hufanyika katika kila wiki ya pili ya mwezi wa Februari kila mwaka kisiwani Zanzibar.

Washiriki hawa hapa chini


Thandiswa (South Africa) Simba & Brown Band (Mozambique)Debo Band (Ethiopia / USA)Ikwani Safaa Musical Club ft Tamalyn Dallal (Zanzibar / USA) Tausi Women's Taarab (Zanzibar)Mari Boine (Norway) Dawda Jobarteh (The Gambia) Del & Diho (Mayotte) Fresh Jumbe & African Express (Tanzania / Japan) Mim Suleiman (Zanzibar / UK) Massar Egbari (Egypt) Nyota Ndogo (Kenya) Obibase (Guinea) Sousou & Maher Cissoko (Senegal / Sweden) Xova (UK) Kunja Dance Theatre (Kenya) Sinachuki Kidumbak (Zanzibar)Isaac Blackman & The Love Circle (Trinidad & Tobago) Bamba Nazar & The Pilgrimage (Suriname / NL) Jimmy Omonga (DRC / NL)Joel Sebunjo & Sundiata (Uganda)Makadem (Kenya) Nass Makan (Egypt) Maureen Lupo Lilanda (Zambia) Juliana Kanyomozi (Uganda) Mzungu Kichaa (Denmark / Tanzania) Jhikoman (Tanzania) Best of WaPi (Tanzania) Shirikisho Sanaa (Zanzibar) Tunda Man (Tanzania) Sosolya Dance Academy (Uganda) Mapacha Africa (Kenya)Swifatui Abraar Group (Tanzania) DJ Eddy (Zanzibar) DJ Yusuf (UK / Zanzibar) Sowers Group (Tanzania) Maia Von Lekow (Kenya) Keita & Swahili Vibes (Zanzibar) Tunaweza Band (Tanzania) KVZ Tupendane (Pemba) and more.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 19, 2009 | | Permalink | Maoni 0

MWANDISHI WA HABARI NA MTANGAZAJI RADIO TIMES FM AJITOSA UCHAGUZI TBF





Selemani Semunyu akirudisha fomu ya kuwania nafasi ya kamishna katika kamisheni ya watoto katika shirikisho la mpira wa kikapu TBF
Semunyu akiwa na wafanyakazi wenzake wa radio Times wakijadili mikakati ya kutoa hamasa katika mchezo wa kikapu.



Mjue Mwandishi wa habari pekee na Mtangazaji wa radio Times Selemani Semunyu aliyejitokeza katika uchaguzi wa Shirikisho la mpira wa kikapu nchini TBF akiwania nafasi ya kamisheni ya watoto jamaa ni mdau wa mpira huo na mchezaji aliyewahi kucheza kikapu katika timu ya Bees ya Tabora,timu ya Shule ya Sekondari ya Uyui, Young Worrios ya Morogoro na Shule ya Sekondari Kigurunyembe ya mkoani humo. hamasa katika kikapu kuendeleza watoto na kuibua vipaji ndio mtazamo na malengo yake ni wakati sasa wa kuchagua viongozi wa ukweli watakao leta tija katika kikapu hasa damu mpya uchaguzi Novemba 28 mwaka huu
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 19, 2009 | | Permalink | Maoni 0

What is the Kiswahili Wikipedia Challenge?

What is the Kiswahili Wikipedia Challenge? This is your opportunity to bring Africa's information online by creating Wikipedia articles in Kiswahili. You can participate by translating English Wikipedia articles into Kiswahili or by writing your own articles from scratch.
You can choose your own topic to write about.
Are you a pursuing a degree in Physics? Translate the entry for 'condensed matter' from English to Kiswahili.
Studying literature? Write an entry on your favorite local author.
Or translate an article about your favorite musician or sports team.
Just think about what topics would be of interest to some of the 100 million Kiswahili speakers worldwide.
Read more about it at: http://www.wavuti.com/4/post/2009/11/kiswahili-wikipedia-competition.html
Subi: wavuti.com
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 19, 2009 | | Permalink | Maoni 0

jukwaa la fiesta one love kwa mbaali

Maandalizi ya ujenzi wa jukwaa la Fiesta One Love unaendelea safi kabisa katika viwanja vya posta, kijitonyama jijini Dar,kama ukilitazama kwa umakini mwana Jamvini nadhani unaanza kupata picha halisi ya jukwaa hilo litakuwa vipi,sio mbaya kama utaamua kwenda kushangaa kimtindo likiishakamilika kabla ya siku yenyewe.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 19, 2009 | | Permalink | Maoni 1

ndiga ya fiesta one love yazidi kuchafuka kwa chata za mastaa

Mratibu wa Miss Tanzania Uncle Hashim Lundenga akiweka saini kwenye gari aina ya Mitsubishi pajero linalotarajiwa kutolewa kwa mshindi wa bahati nasibu kwenye tamasha la Fiesta One Love, itakayofanyika sambamba na tamasha hilo litakalofanyika kwenye viwanja vya posta Kijitonyama, mashabiki watapata nafasi ya kushiriki katika bahati nasibu hiyo kutokana na tiketi zao walizokata ili kuingia kwenye tamasha hilo ambapo wasanii mbalimbali watatoa burudani kutoka hapa nchini na nje ya nchi akiwemo mkali wa Hiphop kutoka nchini MarekaniBusta Rymes.
Mratibu wa Miss Tanzania Uncle Hashim Lundenga akijaribu kutafuta mahali pa kupiga chata lake kwenye gari la bahati nasibu ya Fiesta One love 2009.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 19, 2009 | | Permalink | Maoni 0

kampuni ya zain yainogesha fiesta hisani

Meneja huduma kwa jamii wa kampuni ya simu za mikononi ya Zain Tunu Kavishe akisisitiza jambo kwa watumiaji wa mtandao wa Zain katika kilele cha tamasha la Fiesta one love.
Meneja huduma kwa jamii wa kampuni ya simu za mikononi ya Zain Tunu Kavishe akimkabidhi mtangazaji wa Clouds Fm Ephrahim Kibonde (kwa niaba ya Clouds Media Group),makao makuu ya Zain,kifurushi kama zawadi/hisani kwa ajili ya kuwapa watoto yatima na waishio katika mazingira magumu,huo ukiwa katika mchakato mzima wa kauli mbiu ya FIESTA HISANI,mchakato huo umefanyika jana ikiwa ni sehemu ya kuelekea kwenye kilele cha tamasha hilo.Kampuni ya Zain ni moja ya wadhamini wa tamasha la fiesta one love linalotarajia kufanyika keshokutwa,jumamosi katika viwanja vya posta,kijitonyama jijini Dar.


Meneja huduma kwa jamii wa kampuni ya simu za mikononi ya Zain Tunu Kavishe akifanya mahojiano mafupi moja kwa moja kupitia redio ya Clouds Fm kuhusiana na mchakato mzima wa maandalizi ya Fiesta One Love ikiwa wao ni sehemu ya wadhamini wa tamasha hilo.Tunu alisema kuwa kampuni ya Zain inaijali sana jamii,kwa kulitambua hilo kupitia tamasha la fiesta one love wametoa hisani ya vitu mbalimbali kwa ajili ya watoto yatima na waishio katika mazingira magumu ambavyo hapo baadaye vitakabidhiwa kwa walengwa,aidha aliongeza kuwa mnamo desemba kampuni ya Zain itazunguka Tanzania nzima kwa ajili ya kuendeleza hisani hiyo kwa watoto yatima ili nao wafurahi huku wakielekea kwenye msimu wa sikukuu.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 19, 2009 | | Permalink | Maoni 0

wadau na mastaa wa movie "Baby Powder"













Uzinduzi wa filamu mpya ya Kitanzania "Baby Powder" uliofanyika huko Atlata USA ulifana sana. Habari kutoka Atlanta zinasema kuwa watu kutoka kila kona walijazana katika movie theater hiyo mpya na kisasa.
Ufunguzi huo ulitangulizwa na shughuli ya Red Carpet (Pichani). Ratiba ya onyesho hilo iko kama ilivyopangwa hapo mwanzoni: tarehe 26 Novemba baby powder itakuwa Houston, Texas. Tarehe 5 december itakuwa Washington DC na kufuatiwa na Minneapolis, Minnesota baada ya wiki mbili baadae.
Pichani juu ni wadau na mastaa wa movie wakiwa katika red carpet!! Shukrani ziwaendee watu wote walijitokeza katika onyesho hilo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 19, 2009 | | Permalink | Maoni 0

nani anabishaa?

Wednesday, November 18, 2009
Mtangazaji mwanamichezo mahiri wa Clouds Fm Ephrahim Kibonde akiwa amepozi karibu na kombe la Dunia.!!
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 18, 2009 | | Permalink | Maoni 0

serengeti waing'arisha vilivyo fiesta one love 2009

Watangaji wa Mjengoni Redio Clouds Zamaradi Mketema kushoto na Ephraim Kibonde katikati wakifanya mahojiano mafupi leo asubuhi na Meneja uhusiano wa Serengeti Breweriers Teddy Mapunda (ambao ndiyo wadhamini wakuu) kuhusiana na maandalizi ya tamasha Fiesta litakalofanyika Novemba 21 katika viwanja vya Posta Kijitonyama, kulia ni meneja matukio wa kampuni hiyo Bahati Singh.
Meneja Uhusiano wa Serengeti Breweriers Teddy Mapunda akiweka saini kwenye gari aina ya Mitsubishi pajero linalotarajiwa kutolewa kwa mshindi wa bahati nasibu kwenye tamasha la Fiesta One Love, itakayofanyika sambamba na tamasha hilo litakalofanyika kwenye viwanja vya posta Kijitonyama, mashabiki watapata nafasi ya kushiriki katika bahati nasibu hiyo kutokana na tiketi zao walizokata ili kuingia kwenye tamasha hilo ambapo wasanii mbalimbali watatoa burudani kutoka hapa nchini na nje ya nchi akiwemo mkali wa Hiphop kutoka nchini Marekani
Busta Rymes.

Meneja Matukio na Promosheni wa Serengeti Breweriers Bahati Singh akiweka chata lake kwenye gari la bahati nasibu ya Fiesta One love 2009 mapema leo asubuhi.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 18, 2009 | | Permalink | Maoni 1

MKUU WA MKOA WA TANGA MGENI RASMI MISS utalii 2009 tanga

Washiriki wa shindano la miss utalii Tanga 2009 wakijinoa vilivyo

Mkuu wamkoa wa Tanga Meja Athumani Kalembo, siku ya Ijumaa tarehe 20-11-2009 atakuwa mgeni rasmi katika shindano la kumpata Miss Utalii Tanzania 2009/2010-Tanga. Shindano hilo litakashirikisha jumla ya warembo kumi kutoka wilaya zote za Mkoa wa Tanga, litafanyika katika hoteli ya kitalii ya Tanga Beach Resort.warembo watashindana katika mavazi ya Kitalii, Ubunifu, Kutokea, la Jioni na la Asili.
Mbali ya taji la Miss Utalii Tanga 2009/2010 warembo hao wata wania pia taji la Miss utalii Tanga-Vipaji 2009/2010 kwa kucheza na kuimba nyimbo na ngoma za asili za makabila mbalimbali ya mkoa wa Tanga na Tanzania. Zawadi za fedha taslim jumla ya shilingi milioni tatu na laki tano zitatolewa kama zawadi kwa washindi na washiriki.
Bendi ya Bagamoyo Sound inayo ongozwa na Muumini Mwinjuma itatoa burudani ya muziki wa Dansi, huku upande wa muziki wa kizazi kipya msanii Maunda Zolo na Kasim mganga watatumbuiza.Vikundi mbalimbali vya ngoma za asili vitatumbuiza pia katika shindano hilo la Miss Utalii Tanga 2009/2010.Washindi wa kwanza hadi wa tano na mshindi wa Vipaji watawakilisha Mkoa wa Tanga katika fainali za Miss Utalii Tanzania 2009/2010-Kanda ya Kaskazini, shindano ambalo litajumuisha washindi wa Mikoa ya arusha, Kilimanjaro, Manyara na Tanga.
Washindi nane wa kanda watawakilisha Kanda ya Kaskazini katika fainali za Taifa za Miss Utalii Tanzania 2009/2010. Katika shindano la mwaka huu la Miss Utalii Tanga kiingilio kitakuwa ni shilingi 25,000 / = kwa mtu mmoja, kiingilio hiki kimezingatia ubora na hadhi ya onyesho na shindano la Miss Utalii Tanzania 2009/2010-Tanga Mwaka huu. Waandaaji wa shindano hili ni RAHA ENTERTAINMENT ambao ni mawakala wa waandaaji wenye dhima ya kikomo ya kuandaa na kuendesha mashindano ya Miss Utalii Tanzania kampuni ya Miss Tourism Tanzania Beauty Pageant.
Asante,
AKIDA AHMED JUMAMRATIBU MISS UTALII TANGA>>
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 18, 2009 | | Permalink | Maoni 0

breakfastiiiizzzz


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 18, 2009 | | Permalink | Maoni 6

MEMORIAL SERVICE,WASHINTON DC


Tujumuike na familia ya Elias Stafford Mshana(Massawe) katika ibada jumapili november 22 saa nane mchana(2:00pm) ya kumuombea mama yao mpendwa Bertha Stafford Mshana aliyefariki nov 12/2009 katika hospitali ya KCMC,Moshi Kilimanjaro na kuzikwa november 16/2009,Moshi,Kilimanjaro
Ibada itafanyika Good Samaritan Lutheran Church, 10110 Greenbelt Road, Lanham,Md,20706.Sisi tulikupenda lakini mwenyezi Mungu amekupenda zaidi,ukae katika amani mpaka hapo mwenyezi Mungu atakapo tukutanisha tena,yeye alitoa na yeye ametwaa,jina lake lihimidiwe.
Kwa maelekezo zaidi,wasiliana:

Marco Mbullu 571 426 7124,

Elvis Saria 301 213 0657,

Elias Stafford 301 646 5683

Ray Abraham 301 793 4467
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 18, 2009 | | Permalink | Maoni 0

MISA YA KUMBUKUMBU YA MAREHEMU TOBI aka JIBABA-(MILTON-KEYNES)-

Milton Keynes TZ Society invites you for a prayer to commemorate our beloved Brother,Family & Friend TOBY aka JIBABA ,
Its 3yrs Since His tragic Death, Ceremony will be held on Sat 21st Nov@ Jesus Celeb Centre,Lloyds Court,Central Milton Keynes,MK9 3AT(Formerly Known as Flames)
from 2pm-6pm...
For more info please Contact 07899 784806/07897 362757....
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 18, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Bibi Titi road leo jioni

Tuesday, November 17, 2009

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 17, 2009 | | Permalink | Maoni 0

MABADILIKO YA SIKU YA TAIFA KUPANDA MITI


Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII


TAARIFA KWA UMMA.
MABADILIKO YA SIKU YA TAIFA KUPANDA MITI
Serikali imebadilisha Siku ya Taifa ya Kupanda Miti kutoka Januari Mosi ya kila mwaka na kuwa Aprili Mosi. Mabadiliko hayo yametokanana Waraka wa Waziri Mkuu Na 1 wa mwaka 2009 kuhusu kubadili Siku ya Taifa ya Kupanda Miti kutoka Januari Mosi na kuwa Aprili Mosi ya Kila mwaka.

Kwa mujibu wa waraka huo, kuanzia mwaka 2010 Siku ya Taifa ya Kupanda Miti itaadhimishwa Aprili Mosi ya kila mwaka. Waraka huo unaanza kutumika rasmi tarehe 01 Juni, 2009 na unafuta waraka wa Waziri Mkuu Namba 1 wa Oktoba, 2000.
Uamuzi wa kubadilisha siku hiyo unatokana na mapendekezo yaliyotolewa na Mhe. Jakaya Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Januari Mosi 2008 aliposhiriki maadhimisho ya Siku ya Taifa ya Kupanda Miti na kutaka maadhimisho hayo yahamishiwe kipindi ambacho sehemu nyingi za nchi zitakuwa zinapata mvua.

Kwa mujibu wa waraka huo, Aprili Mosi itakuwa ni siku ya Taifa kuhamasisha upandaji miti huku kila mkoa ukiendelea kujipangia Siku ya Kupanda Miti kutokana na majira ya mvua yatakavyoruhusu. Ili kazi ya kupanda miti iwe inatekelezwa na wadau wote, Waraka huo umeagiza Wizara, Mikoa, Wilaya, Viongozi wa wilaya, Halmashauri za Jiji, Manispaa na Mamlaka za Miji midogo, Tarafa, Kata, Vijiji na mitaa kuandaa programu za utekelezaji mapema iwezekanavyo.

Maafisa Misitu walioko mijini, mikoani, wilayani na vijijini wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu aina ya mbegu na miche inayofaa katika eneo husika na kushauri utayarishaji wa vitalu vya miche kwa wakati unaofaa.

Waraka umemtaka kila kiongozi ahakikishe zoezi la upandaji miti linatekelezwa na kusimamiwa ipasavyo kwenye eneo lake. Aidha, pamoja na masuala mengine kiongozi atapimwa kutokana na juhudi zake za kuhamasisha, kutekeleza na kusimamia wananchi kupanda miti. Halmashauri zote kwa kushirikiana na mamlaka husika, zihakikishe kuwa upandaji miti ni pamoja na kupanda kando kando ya barabara zote nchini.

Waraka huo umetahadharisha kuwa kupanda miti pekee hakutoshi kukabiliana na jangwa kama hatua za makusudi za kutunza na kulinda uoto wa asili hazitachukuliwa. Siku ya Taifa ya Kupanda Miti iliadhimishwa kitaifa kwa mara ya kwanza mwaka 2001 katika eneo la Jangwani mkoani Dar es Salaam.
Ezekiel Maige (Mb)
NAIBU WAZIRI

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 17, 2009 | | Permalink | Maoni 3

miss utalii kinondoni 2009 yazidi kunoga

Wakijiachia ndani ya maji fukwe za COCO Beach mwishoni mwa wikend


Miss Utalii katika pozi
Wamenyooka na wanafaa kuwa mabalozi wa utalii wa ndani,lakini mmoja wao ndiye atakayeibuka na taji la Miss utalii kinondoni 2009.
Washiriki wa Miss Utalii Kinondoni -2009 wakiwa wamejiachia katika mapozi mbalimbali kando kando ya fukwe za COCO Beach, mwishoni mwa wikend.shindano la Miss Utalii Kinondoni linatarajia kufanyika Novemba 20 katika ukumbi wa Msasani Club kinondoni jijini dar.
MWAKA WA NEEMA, WADHAMINI WAZIDI KUMIMINIKA MISS UTALII KINONDONI
Kampuni ya Ele-Tech & Equipment kwa kushirikiana na kampuni ya Tan Country Power Systems ltd za jijini Dar es Salaam, zimejitokeza kuungana na Baadhi ya Makampuni katika kusaidia shindano la Miss Utalii Kinondoni kwa kusaidia masuala mbali mbali yakiwemo mavazi na zawadi kwa Washiriki katika siku ya Fainal.
Aidha kampuni hiyo itagharamia gharama zote za jukwaa litakalotumiwa na warembo siku hiyo,hivyo kufanya jumla ya udhamini wao kuwa wa thamani ya shilingi milioni moja na laki tano (1,500,000).Hatu hiyo imekuja siku ,moja tangu kampuni ya Mashujaa Pub & Entertainment na AL WATER WELL DRILLERS kwa kushirikiana na Kampuni Kubwa kabisa ya Usafirishaji ya Mamaa Sakina Trans zote za Vingunguti kujitokeza pia kudhamini shindano hilo kwa kiasi cha shilingi milioni mbili.
Zaidi ya warembo 17 wamejitokeza katika Mashindano ya Miss Utalii Tanzania 2009/2010 –Kinondoni,ambao wanaendelea na kambi ya mazoezi katika ukumbi wa New Msasani Club Kinondoni Dar Es Salaam chini ya mwalimu wao Ester Kinyunyu ambaye ni Miss Utalii Tanzania 2005/2006 -Iringa.Kuanzia mwishoni mwa wiki hii warembo hao wataanza ziara maalum za kutembelea ,kujifunza na kutangaza maeneo mbalimbali ya kitalii,kitamaduni na kihistoria yaliyopo katika wilaya ya Kinondoni,baada ya jumapili iliyo pita kutembelea kivutio cha ufukwe wa Coco Beach uliopo Oysterbay jijini.
Maeneo watakayotembelea ni pamoja na Kijiji cha Makumbusho Kijitonyama,soko la sanaa za mikono la Mwenge na eneo la biashara la kimataifa la Mlimani City la jijini.Shindano la Miss Utalii Tanzania 2009/2010 – Kinondoni ni mfululizo wa mashindano ya Miss Utalii Tanzania 2009/2010 yanayofanyika katika ngazi mbalimbali za Wilaya,Mikoa na Kanda zote nchini,ambapo washindi wa wilaya hushiriki katika fainali za mikoa,washindi wa mikoa hushiriki katika fainali za kanda na washindi wa kanda watashiriki fainali za Taifa za 2009/2010,huku washindi wa Taifa wakiwakilisha nchi katika mashindano ya dunia ya Miss Tourism World 2009/2010,Miss Heritage World 2009/2010 na Miss United Nations 2009/2010.
Shindano la Miss Utalii Tanzania 2009/2010 –Kinondoni litafanyika siku ya Ijumaa tarehe 27-11-2009 katika ukumbi wa ndani wa kisasa na wa kitalii wa New Msasani Club uliopo karibu na Ubalozi wa Marekani Drive Inn Cinema,Maandalizi yanakwenda vizuri, na litakuwa ni onyesho la karne la nyota tano ambalo litahudhuriwa na viongozi na watu mbalimbali wa mashirika ya umma,binafsi na serikali kitaifa,kimkoa na kiwilaya.
Mkurugenzi wa Ele-Tech & Lihting Agency , Kibo Merinyo, ametaja baadhi ya sababu za kudhamini shindano hili kuwa ni pamoja na kuvutiwa na mfumo mzima wa mashindano ya Miss Utalii Tanzania,ikiwemo wa kuwafundisha washiriki kucheza na kuimba nyimbo na ngoma za asili za makabila mbalimbali ya Tanzania jambo ambalo ni adimu katika mashindano mengine kuonekana.
Wadhamini wengine ni pamoja na Empire Ferniture, Clouds Fm, A-one Tours & Safari, Aurora Security, The Grand Villa Hotel, Mashujaa Pub, Mamaa Sakina Trans, Mlonge By Makai Enterprisess, Daja Saloon, Fitness Centre, Vam General Supply, Mh Idd Azan, New Msasani Klabu, Chicken Hut Tanzanian ltd, Chagga Bite, Savannah Lounge, Kampala International Univarsity(KIU),Michuzi Bllogs & Kitangoma Magazine, Angels Galapo , na Raimbow Social Klabu.
Warembo waliojitokeza na ambao wapo kambini hadi sasa ni Joseline Sekwao,aike Abel,Neema Mashalla,Jackline Mollel,Ratifa Bakari,Christina Masandeko,Zubeda hamisi,Robby Masandeko,Agness Selis,Juliana Johnson,Sauda Ramadhan,Barke Mohamed,Faraja Hassan,Matha Denis,Sarah Shaaban,Lulu Dello,Sophya Dei.
Asante,Shaaban Mpalule
Mkurugenzi Miss Utalii Tanzania,
Wilaya ya Kinondoni
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 17, 2009 | | Permalink | Maoni 2

nikifa njoo unidai !


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 17, 2009 | | Permalink | Maoni 1

TAARIFA YA MSIBA WA MZEE ABUSHIRI KILUNGO


MZEE ABUSHIRI KILUNGO (PICHANI) AMEFARIKI DUNIA USIKU WA KUAMKIA LEO (16/11/2009) NYUMBANI KWAKE TANDIKA,MTAA WA KIVUNGO BAADA YA KUUGUA UGONJWA WA KISUKARI KWA MUDA MREFU.

MAREHEMU KILUNGO AMBAYE ALIWAHI KUWA NAIBU MEYA WA JIJI LA DAR ES SALAAM MIAKA YA NYUMA NA PIA ALIWAHI KUWA MWENYEKITI WA CHAMA CHA SOKA MKOA WA DAR (DRFA).


MAREHEMU KILUNGO AMEACHA MKE NA WATOTO WATANO WATATU WAKIWA NI WA KIUME NA WAWILI WA KIKE.MAZISHI YATAFANYIKA LEO (17/11/2009) SHAMBANI KWAKE TUANGOMA,NJE KIDOGO YA JIJI LA DAR ES SALAAM.
TUNAMUOMBEA KWA MWENYEZI MUNGU AIWEKE ROHO YA MAREHEMU MZEE WETU ABUSHIRI KILUNGO MAHALI PEMA PEPONI
-AMIN
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 17, 2009 | | Permalink | Maoni 2

TANZANIA RED RIBBON CHILDREN'S DAY


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 17, 2009 | | Permalink | Maoni 0

vZAIN BOOM CLUB YAPELEKA WANAFUNZI 20 KATIKA USIKU WA KIPEKEE WA MO-IBRAHIM.

Baadhi ya washindi wa Boom club waliojishindia tickets, wakiwa katikaPicha ya pamoja walipokabidhiwa vitambulisho vyao vya kuingilia katika hafla hiyo Iliyohudhuriwa na marais mbalimbali kutoka Africa
Pichani msanii wa muziki wa kizazi kipya Q-Jay akitumbuiza jukwaani kwenye Boom party hiyo iliondaliwa na kampuni ya simu za mikononi ya Zain mwishoni mwa wikend
Baadaye wanafunzi wa vyuo mbalimbali walikwenda kujiachia Zain Boom Party kwa hisia ndani ya club ya Hunters,Kigamboni jijini Dar
mashindano hayo yalikuwa na na yenye burudisha
Pichani ni wanafunzi wa vyuo mbalimbali wakishindana kucheza mpira wa kikapu katika ufukwe wa bahari ya Hindi kule Hunters Kigamboni jijini dar kwenye party yao ya Boom club iliokuwa imeandaliwa na kampuni ya simu ya Zain mwishoni mwa wikend.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 17, 2009 | | Permalink | Maoni 0

changamka na mtandao wa magari bei poa kabisa



Kwa magari zaidi ya bei poa tembelea http://www.magaribeipoa.com/. pia unaweza kuuza gari lako kupitia hapa bila gharama yoyote,unachotakiwa kufanya ni kujisajilia bila gharama yoyote ili uweze kutuma picha ya gari lako.

Maajenti wa kuuza magari pia mnakaribishwa kutumia mtandao wa magaribeipoa.
NOTE:lugha zinazotumika humu ni mbili,ukitaka kiswahili nenda mpaka mwisho wa page na utaona bendera ya Tanzania,gonga hiyo bendera kwa ajili ya Kiswahili.
Kwa mawasiliano zaidi piga namba hii +255713439707
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 17, 2009 | | Permalink | Maoni 0

MSIBA BOSTON, MA.


MZEE ROBERT L FERUZI
1946-2009
Ndugu, Jamaa na Marafiki, Tunasikitika kuwajulisha ya kuwa Mzee Robert L Feruzi Boston-Masachusetts amefariki dunia siku ya Jumapili [Nov 15th 2009] asubuhi hapa Boston, USA.

Taratibu na mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda Dar es salaam kwa mazishi zinafanyika nyumbani kwake 98 Itasca St, Mattapan, MA
Tunawaomba ndugu zetu mtusaidie kuchangia fedha kwa ajili ya kuwezesha kusafirisha mwili wa marehemu kurudi nyumbani kwa mazishi. Gharama za kuhifadhi mwili, kusafirisha mwili, Jeneza pamoja na gharama zingine ambazo kwa kawaida huja na haya matatizo.

Unaweza kusaidia kutuma mchango wako kwenye Account ya wafiwa kama ifuatavyo:

Innocent E. Lugumamu
BANK OF AMERICA,
ROUTE NUMBER: 011000138
ACCOUNT NUMBER: 004628572563
Address: 12 Walker St, Lowell, MA 01854

IMPORTANT: Kwa wale waliopo nje ya state ya Massachusetts, Out of state deposit circle (zungushia) namba 77, MA. Unapotuma pesa. (Haya ni maelezo muhimu toka kwa bank of America)

Kwa mawasiliano zaidi unaweza kuwasiliana na wafuatao:
Innocent E. Lugumamu 978 996 7690
Steven Buberwa Mutasa 603 320 3220
Crispine Kahabuka 603 261 0802

TUNATANGULIZA SHUKRANI ZETU.

Email-Address: -- ilugumamu@hotmail.com
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 17, 2009 | | Permalink | Maoni 0

ooh bongo foleni.!

Monday, November 16, 2009

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 7

msaada tutani wanajamvini

Wanajamvini kuna mdau ameomba afahamishwe/aelimishwe kuhusu hizi antena za huyu konokono pichani zinamsaidiaje katika maisha yake ya kila siku,tena zinaonekana ziko tatu.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 2

shingo ya upanga ni ipi hapa?


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 1

ajali mbaya imetokea kati ya Mbeya na dar

Kuna taarifa kuwa mabasi mawili yamepata ajali mbaya,moja likitokea Mbeya kwenda Dar maeneo ya milima ya kitonga,inasemekana brake zilifail na inasadikika kuna majeruhi wengi sana,hili basi linajulikana kama Al sayed na basi la pili ni scandnavia lilikua likitokea Dar kwenda Mbeya,limepata ajali likikaribia Makambako junction ya Songea na mbeya,hili halijaua ila dereva ameumia,inasemekana alikua anataka ku-overtake kumbe kuna gari linakuja upande mwingine,akashindwa kushika brake za ghafla na kugonga lori la mizigo.Mwenye taarifa zaidi atuhabarishe na poleni kwa wote.
Habari kwa hisani ya mdau aliyekuwa njiani akija dar.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 0

timu ya tbc yapigwa jeki vifaa vya michezo


Meneja wa timu ya shirika la utangazaji Tanzania TBC SPORTS CLUB Taji Liundi (kushoto katika picha) akipokea msaada wa jezi 20 za juu na chini na mipira miwili kutoka kwa meneja wa uhusiano, habari na mawasiliano wa SERENGETI BREWERIES LIMITED (SBL) Bi. Teddy Mapunda . Msaada huo una thamani ya shilingi laki 8. timu ya tbc kwa sasa ipo TANGA ikishiriki michuano ya SHIMUTTA (shirikisho la michezo kwa mashirika ya umma na makampuni binafsi).
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 0

ziara fupi ya Youssou Nd'our mjengoni Clouds Fm leo mchana

Mwanamuziki nyota wa kimataifa toka nchini Senegal, Youssou Nd'our akizawadiwa fulana na Mkurugenzi wa Clouds Media Group / Prime Time Promotions Bw.Joseph Kusaga mchana huu.
Mkurugenzi wa Clouds Media Group / Prime Time Promotions Bw.Joseph Kusaga akizungumza mchana huu ofisini kwake Mikocheni jijini Dar na Mwanamuziki nyota wa kimataifa toka nchini Senegal, Youssou Nd'our
Youssou Nd'our akiperuzi na kupata uhondo wa mapicha ya nguvu kutoka kwenye jarida bingwa pekeee linalowaenzi wasanii wa hapa nyumbani kwa asilimia kubwa, Kitangoma Magazine ambalo litakuwa mtaani hivi karibuni.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Youssou Nd'our ndani ya choice FM

Mkuu wa vipindi wa Choice Fm ML Chris akiwa amepozi na Youssou Nd'our
Youssou Nd'our akifafanua jambo kwa msisitizo mkubwa kabisa
watangazaji wa Choice Fm Thandy na Baby Kabaye wakizungumza na Youssou Nd'our leo mchana
Youssou Nd'our akifanya mahojiano mafupi leo mchana ndani ya redio ya Choice Fm,pichani ni watangazaji Baby Kabaye na Thandy.Mwanamuziki huyo amesema kuwa amefurahishwa sana na onesho lake la usiku wa kuamkia leo ambalo anakiri wazi kuwa muziki wake unakubalika kwa kiasi kikubwa ikiwemo Tanzania,Youssou Nd'our amesema kuwa anatarajia kurejea tena nchini Tanzania Januari mwakani kwa shughuli maalumu.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 1

Youssou Nd'our ndani ya 88.4

Unaona bwaana,huu ndiyo mpango mzima.! Mtangazaji wa kipindi cha XXL akipeana mkono na Youssou Nd'our kulia kabisa ni Bakari wa Marketing na nyuma kabisa ni Dj Mully B
"Na hii ni studio yetu ya pili ambayo itakuwa ikiendeshwa kisasa kabisa,mara baada ya kila kitu kukamilisha muda mfupi ujao"Sebastian Maganga akimueleza Youssou Nd'our leo mchana
Youssou Nd'our akifafanuliwa jambo na mkuu wa vipindi vya Clouds Fm 88.4 leo mchana Sebastian Maganga,nyuma kabisa ni Reuben Ndege a.k.a Ncha kali
Mwanamuziki nyota wa kimataifa toka nchini Senegal, Youssou Nd'our akiwasili 'mjengoni' leo mchana mara baada ya kupokelwa na Mkurugenzi wa Clouds Media Group/Prime Time Promotions Bw.Joseph Kusaga,Mikocheni jijini Dar.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 0

TIGO CHEMSHABONGO WAKABIDHIWA ZAWDI ZAO.

Kulia ni Deputy HR Manager (Afisa Rasilimali Watu) wa Tigo Bennett Kakorozya akikabidhi zawadi ya Laptop kwa mshindi wa PILI wa promosheni ya TIGO CHEMSHA BONGO Hassan Mohamed wa MBAGALA, katikati ni Tawonga Mpore Ofisa huduma za ziada Tigo na Afisa Uhusiano wa Tigo Jackson Mmbando wakishuhudia wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika leo ofisi za Tigo makao makuu. kushiriki Mteja alitakiwa kutuma neno SWALI kwenda 15550 na kisha alianza kupokea maswali mbalimbali kutoka Tigo kwa mwezi mmoja uliopita.
Kushoto ni Deputy HR Manager (Afisa Rasilimali Watu) wa Tigo Bennett Kakorozya akikabidhi zawadi ya Plasma TV Inch 26 kwa mshindi wa kwanza wa promosheni ya TIGO CHEMSHA BONGO Jamal Jumbe wa KINONDONI, katikati ni Tawonga Mpore Ofisa huduma za ziada Tigo na Afisa Uhusiano wa Tigo Jackson Mmbando wakishuhudia wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika leo ofisi za Tigo makao makuu. kushiriki Mteja alitakiwa kutuma neno SWALI kwenda 15550 na kisha alianza kupokea maswali mbalimbali kutoka Tigo kwa mwezi mmoja uliopita.
TIGO CHEMSHABONGO WAKABIDHIWA ZAWDI ZAO.
WAWILI WATOKA MBAGALA
Tarehe 16 Novemba 2009, Kampuni ya simu za mkoni Tigo leo imekabidhi zawadi kwa washindi wa mchezo wa promosheni ya Tigo Bingwa iliyokuwa ikichezeshwa kwa kipindi mwezi mmoja uliopita

Zawadi zilizokuwa zikishindaniwa katika mchezo huo ni pamoja na 1Plasma TV 26 Inch-LCD mshindi wa Pili ni Laptop DELL na mshindi wa tatu ni Digital camera- SONY.
Washindi waliokabidhiwa zawadi zao wote ni kutoka jijini Dar es Salaam,akiwataja na kuwakabidhi zawadi washindi hao ni JAMAL JUMBE wa KINONDONI 1 Plasma TV 26 Inch, HASSAN MOHAMED wa MBAGALA Laptop VENACE ALEX MSHOBOZI wa MBAGALAambae aliibuka na Digital camera

Promosheni ya Tigo Bingwa Tilizindua tareh 12/10/09 na kufikia kilele chake tarehe 12/11/09. Promosheni hii ilikuwa ni kwa watanzania wote wanaotumia mtandao wa tigo Tanzania
Ili kuingia kwenye mchezo wa promosheni hiyo Mteja alitakiwa kutuma neno SWALI kwenda 15550 na kisha alianza kupokea maswali mbalimbali kutoka Tigo na alipojibu kwa usahihi alijipatia pointi zilizomfanya awe mshindi kadiri alivyokuwa na pointi nyingi

Sisi tigo tunajisikia fahari sana kuendesha promosheni hii ya kipekee kwa kuwa kila mteja wetu alipoamua kushiriki alikuwa akijiwekea lengo la kushinda zawadi anayotaka kutoka kwetu.
Bado Tigo tunaendelea kuwazawadia watanzania walioamua kutumia mtandao wetu kikamilifu kwa kupitia promosheni nyingine ya KWARUZA inayoendelea hivi sasa. hadi sasa tayari tumeshafikisha zaidi ya washindi 230 walioibuka na zawadi za milioni moja, laki tano na laki tatu
Pia ili kuendelea kuboresha huduma za mtandao wa intaneti sasa tunatoa nusu bei kuanzia muda wa saa tano usiku hadi saa mbili asubuhi.
kwa kujiunga na huduma zetu za intanet mteja anatakiwa kutuma neno ALL kwenda namba 15006 na atatumiwa SETTING utakazohifadhi kwenye simu yako na utakuwa umeungwanishwa na mtandao moja kwa moja.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 0

shoo love na Youssou Nd'our

Youssou Nd'our akiwa amepozi na mwanamitindo maarufu hapa bongo Miriam Odemba
Mwanamuziki nyota wa kimataifa toka nchini Senegal, Youssou Nd'our akichit-chat na mmoja wa washabiki wake nyuma ya steji mara baada ya kumaliza onesho lake lililofanyika usiku wa kumkia leo viwanja vya karimjee jijini dar
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 5

mtoto wa mjengoni na nondo yake

Mdau George Njogopa wa Clouds Fm baada ya kula nondozzzz mwishoni mwa wiki katika masuala ya Jinsia katika Maendeleo( Gender Issues in Development) katika chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu J.K.Nyerere Kigamboni zamani (Kivukoni) .
Pichani Njogopa akivalishwa shada la maua na mmoja wa wafanyakazi wa Clousd Media Gropu,Da' Suzzy Bultazar mara baada ya kujinyakulia nondo yake a.k.a stashahada ya masuala ya jinsia katika maendele.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 1

vipaji vinavyoibukia anga ya utangazaji wa mpira

Watangaji wa mpira wa miguu wanaochipukia kwa sasa hapa nchini ENOCK BWIGANE(kulia aliyevaa uzi wa TAIFA STARS)na AHMED SALUM(kushoto)wote wa shirika la utangazaji Tanzania-TBC wakiwajibika katika kutangaza mpira uwanja mpya wa kisasa wa TAIFA jijini DSM.kweli TBC ni shule inayoibua vipaji vipya na vya ukweli katika utangazaji wa mpira nchini.BIG UP TBC na mkurugenzi TIDO MHANDO.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 0

tunajiachia lakini safari bado tunayo kiukweli

Mwalimu, Albert Juakali wa shule ya msingi Iboma iliyopo kijiji cha Udinde Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya akifundisha wanafunzi wa darasa la kwanza chini ya Mti wa Mbuyu kama alivyokutwa na Mpigapicha picha pigapicha picha Brandy Nelson
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 6

Youssou Nd'our V/S Angelique Kidjo walivyoikuna bongo

Youssou Nd'our akiimba kwa hisia jukwaani
Mwanamuziki Angelique Kidjo kutoka nchini Benin akiimba kwa hisia
Mashabiki wakijiwaya mwaya jukwaani safi kabisa
Youssou Nd'our na Angelique Kidjo wakiimba kwa pamoja jukwaani mbele ya umati mkubwa wa watu katika onesho lililofanyika usiku wa kumkia viwanja vya Karimjee.
Youssou Nd'our V/S Angelique Kidjo palikuwa hapatoshi jukwaaani ohoo.
Mwanamuziki nyota wa kimataifa toka nchini Senegal, Youssou Nd'our akitumbukiza kwenye onesho viwanja vya karimjee jijini dar usiku wa kuamkia leo.
Mwanamuziki mwenye asili ya Sudan anayeishi Misri, Emmanuel Jah, akitambulishwa rasmi mbele ya mashabiki kibao na Mwanamuziki nyota wa kimataifa toka nchini Senegal, Youssou Nd'our wakati wa onesho lililofanyika katika viwanja vya karimjee usiku wa kuamkia leo.
"Mzuka ukipanda bwana hauzuiliki hata kidogo"! Pichani ni mwanamuziki nyota wa Kimataifa kutoka nchini Benin, Angelique Kidjo akionesha umahiri wake wa kucheza jukwaani,huku mashabiki waliokuwemo viwanjani hapo walikuwa hawaishi mayowe ya shangwe.
Mashabiki kibao katika viwanja vya Karimjee wakati nyota wa muziki wa kimataifa walipokuwa wakitumbuiza usiku wa kuamkia leo,jijini dar.Onesho hilo ambalo lilifana sana liliratibiwa na kampuni bingwa ya burudani hapa nchini ya Prime Time Promotions Ltd na kudhaminiwa nakampuni ya simu za mikononi ya Zain.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 0

fiesta one love ilivyokuwa ndani ya zenj

Pasha akiwasha moto katika fiesta one love Zanzibar ndani ya ngome kongwe
Baadhi ya mashabiki waliojitokeza katika fiesta one love 2009 Zanzibar
Kikundi cha Stone town kikionyesha umahiri wake wa kucheza nyimbo za mahadhi ya kihindi

Hata akina dada hawakuwa nyuma kuonyesha vipaji vyao vya kujiachia
Alikiba akiwapagawisha mashabiki wake na wimbo wake wa msiniseme
Mashabiki wakijiachia ndani ya fiesta one love 2009 Zanzibar
Chama kubwa Tip Top conection wakiwasha moto ... kutoka kulia ni Tunda Man, Khasim na Madee kifiesta fiesta
Kundi linalopendwa Zanzibar ndani ya Zenji Offside Trick a.k.a Wazee wa samaki wakishoo love
Dj Dr. B akiwasha moto ndani fiesta one love 2009
Kijana machachali aitwaye Wasi kutoka Clouds Tv wakishow love ndani ya fiesta one love 2009 Zanzibar

Baby J akionyesha umahiri wake wa kucheza na kuimba katika fiesta one love 2009 Zanzibar

Michael Jackson bado anakumbukwa Zenji,kama uonavyo pichani msanii kutoka Zanzibar akionesha umahiri wake wa kuyarudi mangoma ya The Wacko jacko ndani ya tamasha la fiesta one love
Kikundi cha vijana machachari kutoka Zanzibar wakitumbuiza jukwaani
Watoto wa Stone town wakionesha umahiri wao wa kucheza katika jukwaa la Fiesta one love 2009 Zanzibar,iliyofanyika mwishoni mwa weekend mjini Ngome Kongwe, ambapo makamuzi hayo yatahamia Kitaifa jijini Daar katika viwanja vya Posta pale Sanyansi kijitonyama.Kama mjuavyo msanii wa kimataifa yupo kama kawa Busta Rhymes atatikisa vilivyo,si ya kukosa mtu wangu.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 0

hafla ya Mo Ibrahim Foundation ilivyofana mliman city

Youssour Nd'our wakiimba kwa pamoja kwa hisia na Angelique Kidjo ndani ya Mlimani City
Rais Jakaya Kikwete na Mo Ibrahim wakisalimiana na mwanamuziki Angelique Kidjo
Ulifika muda wa viongozi wa heshima kuserebuka wakiongozwa na Mh Rais JK
Makofi ya pongezi kutoka meza kuu
Wageni waalikwa wakishangilia huku mikono yao ikiwa hewani
Mwanamuziki wa kimataifa Angelique Kidjo akizungumza mbele ya wageni waalikwa
Mwanamuziki Lady Jay Dee jukwaani akiwatumbuiza wageni waalikwa sambamba na skwadi lake zima ndani ya ukumbi wa mikutano wa Mlimani City mwishoni mwa Wikend
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 1

mnuso wa thanksgiving tanzania hostoun


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 0

washiriki wa miss east africa 2009 kuanza kuwasili desemba 1



SEFORA MESSELE GHEBREEZGABIHEIR-18 YEARS (ERITREA)


REBEKA GETACHEW-23 YEARS (ETHIOPIA)
SELAMAWIT ZERABRUCK GHEBRESLASSIE -18 YEARS (ERITREA)
MARRY KIRABO -18 YEARS (UGANDA)
ALIDA GROLIA KANEZA-19 YEARS (BURUNDI)
QUEEN BELLE MONIQUE-23 YEARS (BURUNDI)
AKAZUBA CYNTHIA-20 YEARS (RWANDA)

AKAZUBA CYNTHIA -20 Y(L)and MAHORO ANNET-23 Y (R)(RWANDA)


Warembo wanaoshiriki mashindano ya kimataifa ya MISS EAST AFRICA 2009 wataanza kuwasiri Nchini tarehe moja mwezi ujao kwa ajili ya mashindano hayo yanayosubiliwa kwa hamu kubwa na watu wengi Barani Afrika.
Wakiwa jijini Dar es salaam, warembo hao watafikia katika hoteli ya kimataifa ya Kunduchi Beach Hotel & Resort ambayo ndiyo hoteli rasmi ya mashindano ya Miss East Africa 2009.

Mashindano ya MISS EAST AFRICA 2009 yanatarajiwa kufanyika tarehe 18 mwezi ujao katika ukumbi wa Mlimani City jijini dare s salaam na yatawashirikisha warembo kutoka Nchi 14 za ukanda wa Afrika mashariki ambazo ni pamoja na wenyeji Tanzania,
Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.
Nchi zingine zinazoshiriki katika mashindano hayo ni Ethiopia, Eritrea, Djibouti, Somalia, pamoja na visiwa vya Seychelles, Comoros, Madagascar, Reunion na Mauritius.
Mashindano hayo yanayoandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Limited ya jijini Dar es salaam yanatarajiwa kutizamwa na watu zaidi ya millioni 200 kupitia katika Television barani Afrika.
Mrembo Claudia Niyonzima wa Burundi ndiye anayeshikilia taji la Miss East Africa kwa sasa.
Rena Callist,
Chairman,
MISS EAST AFRICA PAGEANT

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 1

Braza Mathew alivyomeremeta na Veronica Martin

Maharusi wakiwa katika nyuso za furaha kabisa
Bibi harusi Veronica akiwa amepozi na dadazz.
Maharusi wakiwa wamepozi katika picha ya pamoja ya kakazz na mashemejizz
Maharusi wakiwa wamepozi na wapambe wao safi kabisa
Maharusi wakiserebuka ukumbini
Maharusi wakiserebuka na wageni waalikwa ukumbini kwa furaha kabisa.Blog ya JIACHIE inawatakia Maisha mema na marefu katika jahazi lenu jipya la maisha ya ndoa,pia Mungu awabariki sana kwa ushirikiano mlionipa katika kuifanikisha shughuli hii.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 0

maharusi na wapambe wakimenyuka

Bibi harusi veronika martin akiwa amenaswa katika pozi hili mwanana sana
Raha ya kula nikulishe kwa maharusi
Maharusi na wapambe wao wakiwa katika kiota chao wakijichana vilivyo
Maharusi wakifanya Cheerzzz kwa pamoja.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 1

raha ya keki kwa maharusi

Bwana harusi akikabidhi keki kwenye meza ya wakwe zake waliomzalia chema
Bibi harusi akikabidhi keki kwenye meza ya wakwe zake kwa heshima na unyenyekevu
Bibi harusi na mpambe wake wakipeleka keki kwenye meza ya wakwe.
Bibi harusi veronika akimlisha keki ya upendo mumewe Mathew kwa unyenyekevu
Maharusi wakikata keki yao ya upendo ukumbini huku umati wa wageni waalikwa wakishuhudia tukio hilo adhimu.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 0

mila ina sehemu yake pia katika harusi

Maharusi wakipata kinywaji cha kimila kabla hawajaingia ukumbini
Mila kwanza ilipewa kapau mbele kama uonavyo pichani.
Maharusi wakiwasili ukumbini na kupokelewa na wazazi wa pande zote mbili
Mwishoni mwa wiki Braza Mathew Maiko alifunga ndoa takatifu na mkewe Veronika Martin katika kanisa la St Josph na baadaye mnuso wake kufanyika kwenye ukumbi wa Banola,Mwenge jijini Dar.Pichani ni sehemu ya maharusi na wapambe wao walipokuwa wameketi.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 16, 2009 | | Permalink | Maoni 4
Idadi ya watu