Sunday, May 26, 2013
Saturday, May 25, 2013
TASWIRA WAKATI WA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA AU JIJINI ADDIS ABABA, ETHIOPIA
Marais wastaafu waliohudhuria maadhimisho ya miaka 50 ya AU katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addid Ababa, Ethiopia. Kutoka kushoto ni Dkt Kenneth Kaunda (Zambia), Sam Nujoma (Namibia) na Mzee Festus Mogae (Botswana)
Mama Salma Kikwete na wake wa marais wengine wakiwa katika mkutano wa maadhimisho ya miaka 50 ya AU katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addid Ababa, Ethiopia
Wapiga picha toka nchi mbalimbali wakiwa kazini wakati wa mkutano wa maadhimisho ya miaka 50 ya AU katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addid Ababa, Ethiopia.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoka katika chumba cha mikutano baada ya kuhudhuria kikao cha 29 cha wakuu wa nchi za NEPAD pembeni ya mkutano wa maadhimisho ya miaka 50 ya AU katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addid Ababa, Ethiopia.
Wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika na wageni mashuhuri walioalikwa wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mkutano wa maadhimisho ya miaka 50 ya AU katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addid Ababa, Ethiopia.PICHA NA IKULU
TASWIRA MBALIMBALI ZA MAKAO MAKUU YA UMOJA WA AFRIKA JIJINI ADDIS ABABA WAKATI WA KUADHIMISHA MIAKA 50 YA UMOJA HUO
Wajumbe, wageni waalikwa, wanahabari na wadau mbalimbali wakijichanganya nje ya ukumbi wa mkutano wakati wa mapumziko
Viongozi wa nchi mbalimbali waliohudhuria
Mandhari za nje na ndani ya jengo la Makao Makuu ya Umoja wa Afrika jijini Addis Ababa, Ethiopia
![]() |
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mhe Ban Ki Moon akiwa meza kuu pamoja na Rais wa AU Mama Nkosazana Dlamini Zuma na Waziri Mkuu wa Ethiopia Mhe. Hailemariam Desalegn na viongozi wengine wa umoja huo
|
Sehemu ya ukumbi wa mikutano kwa ndani.PICHA NA IKULU.
USAHIRI WA SHINDANO LA BIBI BOMBA WAFANYIKA LEO KWENYE VIWANJA VYA LEADERS CLUB, TAMASHA LA NYIMBO ZA MAKABILA LINAENDELEA
Majaji wa Shindano la 'Bibi Bomba' kutoka (kushoto) Zamaradi Mketema, Babuu wa Kitaa, Regina Mwalekwa na Benny Kinyaiya, wakifuatilia washiriki wakati wakijieleza kuhusu ufahamu wa shindano hilo, lililoanza leo katika Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, wakati wa Tamasha la Nyimbo za Makabila 'Tamadunika' linaloendelea hivi sasa viwanjani hapa.
Mmoja kati wa washiriki 32, akijieleza wakati wa mahojiano rasmi viwanjani hapo....
Mmoja kati wa washiriki 32, akijieleza wakati wa mahojiano rasmi viwanjani hapo....
Baadhi ya wanacrew wasimamizi wa shoo hiyo, wakiwa eneo la tukio.....
Babu wa Kitaa, (kushoto) akiburudika kwa miondoko ya sebene na mmoja wa washiriki wa shindano hilo.
Sehemu ya washiriki waliojitokeza kushiriki shidano hilo...
Madabida mgeni rasmi Tamasha la wasanii chipukizi la Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA)
MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida atakuwa mgeni rasmi katika tamasha la Mastaa chipukizi zaidi ya 320 litafanyika Jumapili 26, 2013 katika ukumbi wa Starlight Hotel kuanzia saa 4 asubuhi.
Peter Mwenda |
Mwenyekiti wa Shiwata, Caasim Taalib alisema Madabida ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) atapata nafasi ya kuona vikundi mbalimbali vya sanaa kikiwepo kikundi cha Kaole, Splendid, Super Shine Taarab pamoja na wasanii mbalimbali wa Bongo Flava, Maigizo,Ngoma, Dansi na Sarakasi nao wamethibitisha kushiriki.
Taalib alisema wasanii wakongwe wa bongo flava walioalikwa ni Stara Thomas, Safi Theatre Group, Ommy G na waigizaji wakongwe wa Kaole na Splendid wataonesha umahiri wao katika fani ya sanaa Kauli Mbiu ikiwa ni Kilio cha Msanii .
Vikundi vingine vitakavyonesha vipaji vyao ni Kepteni Shaibu, Tanzania Disabled, Uyoga Boga Village, Ndafu Arts Group, CGC, Magengistar Crew, Dodo Arts Group, Culture Arts Group, Wachapa Kazi Academy, Soweto Picture, Shiwata Commedy, Mwavionelachi, Manuari Arts Group, Tandale Morden Taarab na Begeja Wushu,
Taalib alisema tamasha hilo ambalo limepata kibali cha Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pia wamealikwa Shirikisho la Sanaa za Maonesho Tanzania,Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF),Shirikisho la Muziki Tanzania na Shirikisho la Sanaa za maonesho Tanzania.
Mwenyekiti aliwaomba viongozi wengine wa bendi za muziki, taarab, vikundi vya sanaa,mapromota,maprodusa na wadau wote kushiriki katika tamasha hilo ili kujenga ushirikiano wa pamoja.
Issere Sports yatoa jezi, mipira kwa vijana Kondoa
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Isere Sports, Abbas Ally Isere (kulia) akimkabidhi jezi seti moja mwakilishi, Dige Shaaban Nkusa kwa ajili ya timu ya vijana wa kijiji cha Mwembeni wilayani Kondoa ili kuimarisha michezo vijijini.
======= ===== ======
KAMPUNI ya Isere Sports imetoa vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh. mil. 1.7 kwa ajili ya kuendeleza vijana katika wilaya ya Kondoa.
Akikabidhi vifaa hivyo jana, Mkurugenzi wa Masoko wa Isere Sports, Abbas Isere alisema ametoa vifaa hivyo ili kuwasaidia vijana kupenda michezo ili kujenga afya na kujikinga na vitengo cha kihalifu.
Abbas alisema vifaa alivyotoa ni kwa ajili ya vijiji vya Changaa kwa Mafunchi ambako wamepewa jezi, mipira na soksi, katika kijiji cha Mwembeni kata ya Hondomairo wilayani Kondoa wamekabidhiwa vifaa kama hivyo.
Akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya vijana wa Changaa, Issa Lubuva alisema umefika wakati kwa wananchi waishio mijini kuwakumbuka vijana waliobaki nyumbani kwa kuwapatia vifaa vya michezo.
Naye Dige Shaaban aliyepokea vifaa kwa niaba ya kijiji cha Mwembeni alisema wachezaji wengi wapo vijijini lakini hawajapata fursa ya kuonesha vipaji vyao hivyo vifaa hivyo vitasaidia kutoa wachezaji kutoka wilaya ya Kondoa.
RAIS KIKWETE KATIKA MKUTANO WA SHEREHE ZA MIAKA 50 YA AU JIJINI ADDIS ABABA LEO
Rais Jakaya Mrisho Kikwete Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya AU katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013.
Muono wa jicho la samaki katika Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya AU katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013
Marais Wastaafu wakiwa katika Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya AU katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013
Viongoi AU wakiwakumbuka waliotangulia mbele ya haki.PICHA NA IKULU
MKUTANO WA VIONGOZI WA MATAWI YA VYUO YA CCM WAFANYIKA JIJINI DAR LEO.
Kaimu Mwenyekti vyuo vikuu, wilaya ya Dar es salaam, Assenga Abubakar (Kushoto),Katibu Msaidizi Mkoa wa vyuo vikuu,anayeshughulikia na mikoa ya Dar es salaam na Zanzibar na Kepteni mstaafu,Alhaji Mohamed Ligola wakiwa kwenye mkutano na viongozi wa matawi ya vyuo ya CCM DSM.
Baadhi ya viongozi wa matawi ya CCM ya vyuo vikuu mkoa wa Dar es salaam wakiwa kwenye mkutano wao ambao pamoja na kujadili masuala mbali mbali ya kisiasa na masaula ya gesi Mtwara pia walipata wasaa wa kupata Darasa la Itikadi.
DADA SILVIA ANAFUTA MCHUMBA KUANZIA MIAKA 35-40
Habari kaka Michuzi, nimekuwa nikiona wenzangu wanafanikiwa kupata wachumba na hatimaye ndoa kupitia blogu yako. Naomba na mimi uniwekee tangazo langu ndugu yangu, naitwa Silvia natafuta mchumba mwanaume ambaye yupo makini, mpole, na aliye tayari kuanzisha familia. Asiwe malaya, asiwe na watoto, asiwe na mke wala ambaye hajawahi kuoa, awe mkristo na pia awe na elimu ya chuo kikuu. Umri wake kuanzia miaka 35 mpaka 40.
Napatikana kwenye email address:
Asante kaka Michuzi
Rais Kikwete awasili Addis Ababa kuhudhuria sherehe za miaka 50 za umoja wa nchi za afrika (AU)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole jijini Addis Ababa alipowasili Ijumaa usiku tayari kujiunga na viongozi wenzie wa nchi za Afrika katika sherehe za miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa nchi za Afrika (AU) zinazofanyika leo katika makao makuu ya umoja huo
Rais Kikwete, Mama Salma Kikwete wakiwasili Addis Ababa
Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakipata maelezo ya maandalizi ya sherehe hizo toka kwa balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Profesa Joram Biswaro mara baada ya kuwasili Addis Ababa.PICHA NA IKULU.
========= ====== ======
========= ====== ======
Rais Jakaya Mrisho Kikwete ni miongomi mwa marais wa bara la Afrika watakaohudhuria Sherehe za kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa nchi za Afrika (AU) zinazo fanyika rasmi leo Jumamosi Mei 25, 2013 katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Shamrashamra zimetawala kila pembe ya jiji la Addis, wakati viongozi wa nchi za Afrika wakiwasili mmoja baada ya mwingine katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Bole.
Muungano wa Afrika wakati huo ukijulikana kama OAU, ulizaliwa Mnamo Mei 25, 1963 jijini Addis Ababa, ukianza na nchi za 32 na baadaye nchi 21 zikajiunga miaka ilivyozidi kwenda, huku Afrika ya kusini ikijiunga kuwa mwanachama wa 53 mwaka 1994.
Mwaka 2001 OAU iligeuzwa kuwa AU katika mkutano uliofanyika Lusaka, Zambia. Jumamosi hii kutakuwa na sherehe za kilele kuadhimisha miaka hiyo 50 ya AU na kuhudhuriwa na marais karibia wote wa Afrika.
Kauli mbiu ya sherehe za hapo kesho ni mjadala mkuu kuhusu ushirikiano wa nchi za Afrika na kuimarishwa kwa muungano huo. Mwenyekiti wa tume ya muungano huo, Dr Nkosazana Dlamini Zuma, anaseme kuwa hii itakuwa fursa kwa AU kujadili kuhusu uwezo wa bara hili na ambacho kinaweza kufikiwa katika miaka 50 ijayo
Kupinga Kwangu Ubaguzi Kulinifanya Niandamwe Na Vikundi Vya Kibaguzi Ulaya
Ndugu zangu,
Kufuatia vurugu za vijana na polisi, zinazoendelea kwenye viunga vya Stockholm, Sweden, juzi hapa nilisimulia ushiriki wangu kwenye Kamati ya Kitaifa ya watu 12 nchini Sweden iliyoandaa rasimu iliyopelekea kuundwa kwa kituo cha kwanza cha kitaifa dhidi ya ubaguzi nchini Sweden.
Ilikuwa mwaka 2003. Kazi hiyo ilipelekea wajumbe wote 12 kuandamwa na vikundi vya kibaguzi si tu katika Sweden, bali Ulaya pia. Hata hivyo, hatukukata tamaa. tuliifanya kazi hiyo hadi mwisho. Hapa chini ni moja ya taarifa za moja ya vikundi hivyo vya kibaguzi ambapo jina langu pia limeorodhoshwa...
Message 174
From: Antiracist Laponia
Subject: CETRUM MOT RASISM, CMR like a copy of fake antiracist league NMR (...like a kind
CETRUM MOT RASISM, CMR like a copy of fake antiracist league NMR... Soma zaidi..http://www.mjengwablog. com/habari-za-kijamii/item/ 2897-kupinga-kwangu-ubaguzi- kulinifanya-niandamwe-na- vikundi-vya-kibaguzi-ulaya. html#.UZ_O3Mrwnqo










.jpg)







































